
Shetta akimtambulisha baunsa wake, anaitwa Mbrazili
Sherehe hiyo ambayo iliambatana na uzinduzi wa management ya Shetta, ilipambwa na mastaa mbalimbali wa muziki, filamu pamoja na wadau wa sanaa ya muziki.
Akizungumza na waandishi wa habari akiwa katika sherehe hiyo iliyofanyika katika ukumbi wa Rouge Hyatt Recency Hotel, Jijini Dar es salaam, Shetta alisema ameamua kufanya hivyo ili kuwashukuru wadau mbalimbali waliomsaidia kumfikisha hapo alipo.
“Kusema kweli Shetta amekuwa na safari ndefu katika maisha yake ya muziki, lakini haya mafanikio yamekuja kwa michango ya watu wengi sana, media, mashabiki pamoja watu wangu wa karibu. Kwa hiyo nimeona bora niwaite hapa ili tujipongeze kwa hapa tulipofikia, kwa sababu haikuwa kazi rahisi. Hapa nimewaalika watu mbalimbali pamoja na mashabiki wangu ili waje na wao kufurahia hapa nilipofikia, kwa hiyo tutakumwa na kula pamoja,” alisema Shetta.
Pia Shetta aliweza kutambulisha management yake mpya, baunsa wa kumlinda pamoja na dancer. Angalia picha.

Shetta akitambulisha management yake mpya ikiongozwa na Michael Mligwa aka MxCarter (wakati kati)

Idris akiongea na waandishi wa habari

Idris Sultan

Irene Uwoyo

Linah akiwa katika pozi

Mashabiki wa Shetta wakisikiliza jambo kwa makini

Master Jay akiwa na Alawi Junior

Shaa

Shetta na Barnaba

Shetta akimtambulisha baunsa wake

Shetta akiwa na Gadner

Shetta akiwa red carpet

Shetta akiwasili eneo la tukio

Shetta akiwatambulisha dancer wake

Shetta akizungumza



















No comments:
Post a Comment