Monday 19 September 2016

Mchekeshaji Kevin Hart amerudi kwenye game ya muziki?

Najua wengi mtakuwa mnamfahamu mchekeshaji mkubwa na maarufu duniani kutokea Marekani Kevin Hart, amezikamata headlines kwenye mitandao mbalimbali kwa uamuzi wake wa kurudi kwenye Game ya muziki wa Hip hop ambapo apo awali alisitisha na kujikita kwenye fani ya uchekeshaji zaidi.

Kituo kikubwa cha Marekani Enewskimeripoti kuwa Kevin Hart  a.k.a Rapper Chocolate Droppa jina analolitumia kimziki ambapo Leo September 19 2016 ameachia single iliobeba jina “Baller Alert” chini ya studio Motown Records za Marekani.

rs_640x962-160914160506-640-kevin-hart-chocolate-droppa-bn-091416

Zaidi anatarajia pia kutoa mixtape yake ya What now? atakayoiachia Oct 7, pia nakusogezea video Kevin Hart a.k.a Chocolate Droppa akiwa ana chana free style, itazame hapa chini mtu wangu


No comments:

Post a Comment