Kitu cha mwisho kimegusa headlines kuhusu mwanariadha wa South Africa, Oscar Pistorius ilikuwa ishu ya kuachiwa kutoka gerezani na kutumikia kifungo akiwa nyumbani kwa mjomba wake, Pretoria.
Mambo huenda yakabadilika, mashtaka ya Oscar Pistorius yamerudishwa tena Mahakamani ambapo safari hii kesi inabadilishwa na waendesha mashtaka wametaka hukumu yake iwe ya mauaji ya kukusudia na sio ya mauaji ya bahati mbaya.
Oscar Pistorius tayari amekaa jela mwaka mmoja katika hukumu ya miaka mitano aliyopewa kabla ya kuhamishiwa kuendelea na hukumu ya kifungo cha nyumbani ambacho anatumikia nyumbani kwa mjomba wake, Pretoria.
Kwa mashtaka mapya yanayomkabili huenda kifungo chake kikafikia mpaka miaka 15 jela badala ya ile mitano aliyohukumiwa.

No comments:
Post a Comment