Friday, 8 May 2015

MAJANGA MWAKA HUU

Januari 13: Ajali ya treni ya Mizigo ilitokea maeneo ya stesheni ya Pugu Mpiji mabehewa matatu ya treni ya hiyo iliyokuwa ikitoka Dar es Salaam ikielekea Bara yaliacha njia na moja kuanguka.

Februari 19: Watu wawili walikufa papo hapo huku wengine 45 wakijeruhiwa baada ya basi la abiria la Kidia lililokuwa likitokea Dar es Salaam kwenda Mwanza kugongana uso kwa uso na lori katika kijiji cha Vikonje wilayani Chamwino mkoani Dodoma.

Aprili 17: Watu 38 walipoteza maisha katika matukio mawili tofauti, likiwamo la ajali ya basi dogo aina ya Toyota Hiace iliyoua watu 19 wakati ikifanya safari ya wizi mkoani Mbeya.

Aprili 12: Watu 18 waliteketea kwa moto baada ya basi la Kampuni ya Nganga Express na lori aina ya Fuso kugongana uso kwa uso na kuwaka moto katika eneo la Iyovi, Milima ya Uduzungwa, Morogoro.

Machi 3: Watu 38 walifariki dunia na wengine zaidi ya 60 kujeruhiwa vibaya kufuatia mvua kubwa ya mawe iliyonyesha usiku kucha na kusababisha mafuriko katika Kijiji cha Mwakata, Kata ya Isaka Wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga.

Aprili 6: Watu watano walifariki dunia papohapo katika kijiji cha Shilabela, kata ya Bwanga wilayani Chato, Geita baada ya kupigwa na radi wakati wakiendelea na ibada ya Sikukuu ya Pasaka.

Mei Mosi: Watu wanaoshukiwa kufanya vitendo vya ugaidi walilipua bomu na kusababisha watu watano kujeruhiwa wakati wakitoka kwenye maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi katika Kijiji cha Msolwa Ujamaa, kilichoko Kata ya Sanje wilayani Kilombero

Mei 4: Mgomo wa madereva nchini kote ambao kwa mara ya kwanza ulisababisha mabasi yote kutoka Dar es Salaam kwenda mikoani na nchi jirani kushindwa kuondoka.

No comments:

Post a Comment